Enter Adress
Saturday, November 24, 2012
Friday, November 23, 2012
Friday, November 9, 2012
HIKI NDICHO NILICHO KIGUNDUA KWENYE UCHAGUZI WA URAIS WA MAREAKANI
TUANZE NA PENZI , KWENYE MAFANIKIO HUWA PENZI LINA CHANUA KAMA UNAVYO JIONEA
KWA UPANDE WA FAMILIA
NA HAWA NI WAFUASI WA OBAMA
KWA UPANDE WA ROMNEY HALI ILIKUWA HIVI
NA KWA UPANDE WA FAMILIA YA MR ROMNEY HALI ILIKUWA HIVI
NA HAWA NI WAFUASI WA ROMNEY
Wednesday, November 7, 2012
Monday, November 5, 2012
HATA KAMA TUNATOFAUTIANA KIMAWAZO KUPONGEZANA NI KITU KIZURI
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni
na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe kwa hotuba nzuri ya kumkaribisha na
kumsifia kwa kazi anayofanya katika maendeleo ya miundombinu nchini katika eneo
la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai.
Thursday, November 1, 2012
Tuesday, October 30, 2012
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Bw.
Prashant Patel (katikati) akizungumza wakati wa uzinduzi wa tovuti itakayokuwa
inajulikana kama www.misstanzaniatreasures.com
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Wengine katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa tovuti hiyo, Bw. Ali Zoeb
(kushoto) na mshauri wa habari wa tovuti hiyo, Bw. Peter Keasi.
MISS TANZANIA YAZINDUA TOVUTI YASISITIZA UMUHIMU WA UREMBO
Jamii imesisitizwa
kuona shughuli za urembo kama fani nyingine ambayo ikifanywa vizuri inaweza
kumkomboa mshiriki kiuchumi na kumuibua kama mtu wa muhimu katika jamii.
Wito huu umetolewa
na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Bw. Prashant Patel aliyekua mgeni
rasmi katika uzinduzi wa tovuti ya mashindano hayo, www.misstanzaniatreasures.com,
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
“Lengo la tovuti hii ni kutaka kueneza
elimu hiyo na kuonyesha kwamba urembo ni kazi au fani kama nyingine na wala
haina uhusiano wowote na uhuni kama baadhi ya watu wanavyoendelea kuamini,”
alisema Bw. Prashant.
Alisema wengi wa warembo waliowahi
kufanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania leo hii ni watu wenye mafanikio
makubwa, kila mtu akifanya kile anachokipenda na kukiweza.
Alisema tovuti hiyo inataka kuwaibua siyo
tu washindi wa Miss Tanzania waliopita, bali washiriki mbalimbali waliwahi
kushiriki katika mashindano hayo na kuonyesha wako wapi, wanafanya nini, ndoto
na matarajio waliyonayo na hata changamoto wanazokumbana nazo.
Hadi sasa kuna jumla ya washiriki zaidi ya
elfu tano tangu Miss Tanzania ianzishwe mwaka 1994.
Alisema kamati ya MissTanzania inaamini warembo
hawa ni hazina na hivyo wanataka kuonyesha hazina iliyopo katika taifa.
Alisema juhudi hizi za kuanzishwa kwa
tovuti hii zitafuatiwa na uanzishwaji wa jarida litakalojulikana pia kama Miss
Tanzania Treasures.
Akielezea zaidi alisema sehemu ya faida
itakayotokana na tovuti hii na jarida hilo itatumika katika kuchangia maendeleo
ya warembo hawa kama elimu na shughuli mbalimbali wanazofanya kwa utaratibu
utakaopangwa. Pia, faida itakayopatikana
itatumika katika kusaidia watoto yatima hapa nchini.
“Tovuti hii itasaidia dunia nzima
kushuhudia na kujua kwa undani kuhusu Miss Tanzania. Hii ni fursa nyingine katika kukuza sekta ya
utalii hapa nchini maana hakuna ubishi kwamba Miss Tanzania imekua moja ya njia
za kukuza utalii wetu nje ya nchi,” alisisitiza.
Akielezea zaidi alisema tovuti ni njia
muafaka katika kipindi hiki cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
ambapo maendeleo yanategemea zaidi ufanisi katika mawasiliano.
“Tovuti hii itasaidia kujenga mtandao baina
ya warembo wenyewe na wakajua jinsi ya kushirikiana katika maswala mbalimbali
ya kijamii na kiuchumi na hivyo kuchochea maendeleo,” alisema.
Alisisitiza kuwa tovuti hii pia itasaidia
kujenga mahusiano na mawasiliano kati ya warembo wa Miss Tanzania kwa upande
mmoja na wadau wa maendeleo ndani na nje
ya nchi.
“Tutawashirikisha wadau mbalimbali katika
swala hili muhimu na ni wito wetu kwamba wasituangushe kwa faida ya nchi yetu,”
alisema Bw. Prashant.
Kwa upande wake, Mkurugenzi
Mtendaji wa tovuti hiyo, Bw. Ali Zoeb aliwaahidi warembo walioshiriki uzinduzi
huo kuwa tovuti hiyo itasaidia sana katika kuwaunganisha na wadau mbalimbali
ndani na nje ya nchi na kuwasisitiza warembo popote walipo kuanza kujenga
mazoea ya kutembelea tovuti hiyo na kujua kinachojiri.
Naye, mshauri wa
habari wa tovuti hiyo, Bw. Peter Keasi alisema tovuti na jarida
litakaloanzishwa hivi karibuni vitasaidia kurahisisha mawasiliano kufanya kazi
kama daraja baina ya warembo hapa nchini, jambo alilosema ni muhimu kwa
maendeleo.
Uzinduzi huo
ulishuhudiwa na warembo walioko kwenye kambi ya Miss Tanzania kwa sasa pamoja
na wadau wengine wa urembo hapa nchini.
Mwisho
Friday, October 26, 2012
NAIBU WAZIRI AELEZA KILICHOMFANYA KUSEMA TANZANIA NI MUUNGANIKO WA ZIMBABWE NA PEMBA
Naibu Waziri Philipho Mulugo
Kuanzia
juzi taarifa na video ya Naibu Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi wa
Tanzania Philipo Augustino Mulugo zimeanza kusambaa kwa watanzania wengi
kuhusu alichosema akiwa Afrika Kusini kwenye mkutano wa kimataifa
kwamba Tanzania ni muungano wa visiwa vya bahari ya Hindi, Pemba na
Zimbabwe.
Mulugo
leo amezungumza na Power Breakfast ya CLOUDS FM na kusema kabla ya yeye
kupanda kuanza kuzungumza kulikua na kiongozi wa Zimbabwe ambae alitoka
kuzungumza na nina mkariri akisema
“sasa
ilibidi lazima baada ya kufika pale ni lazima umshukuru mwenzako
aliepita sasa kama mawazo ndiyo yaliyokua yamedhania hivyo kwamba basi
hapa naitamka Zimbabwe kwa sababu zote zimeanzia na Z labda ilitokea
hivyo lakini nakiri kabisa kwamba sikua na makusudio kwamba naitamka
Zimbabwe lakini kule kwenye power presentation inaonekana kabisa
ukifungua pale ni Tanzania imeungana na Zanzibar Pemba na Tanganyika
kama ambavyo tunajua kwa sababu ile ni historia hakuna asiejua hata
mtoto wa darasa la tatu”
“Niseme
tu kwamba hiyo ni kuteleza kwa ulimi na nilikua namfikiria yule waziri
wa Zimbabwe kwa sababu alikua ametoka kuhutubia kabla ya mimi, nilikua
naomba ieleweke hivyo…………
na
wengi wameongea wanahoji lugha kiingereza, jamani tukubaliane kwamba
kusema Zimbabwe badala ya Zanzibar sidhani kama inaendana na drama
yenyewe kwa sababu mimi nimekua mwalimu mda mrefu nimefundisha wanafunzi
wangu na wananifahamu uwezo wangu mkubwa na tena mimi ni mwalimu wa
historia hata degree yangu ni mimi ni mwalimu wa historia na Economics,
labda
niliongea nilikua sijielewi na ningegundua nimetamka Zimbabwe ningeweza
kuomba radhi, mataifa yote wawe waafrika wawe wazungu wengi huwa
tunazingatia kuangalia kwenye power point pale, wengi huwa hawasikilizi
sauti” – Mulugo
Kuhusu
kukosea kutaja mwaka, Namkariri naibu waziri akisema “mimi pale nia
yangu ilikua ni kusoma namba moja moja nikashtukia nakwenda kusoma
mbili, haijakaa kama nimekosea kiingereza kama watu wanavyoipanua kwa
mfumo huo lakini kama watu wamenielewa hivyo niombe tu msamaha”(SOURCE djfetty.blogspot.com)
Subscribe to:
Posts (Atom)