Enter Adress

Wednesday, October 17, 2012

JK AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA MKOANI PWANI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Kikwete ameweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya Msata – Bagamoyo na kuwataka  wakazi wa mkoa wa Pwani kutumia fursa zinazotokana na barabara hiyo kujiletea maendeleo.
Rais Kikwete amesema barabara hiyo itakapokamilika ujenzi wake kwa kiwango cha lami itafungua milango ya biashara kwa wakazi wa mkoa wa Pwani pamoja na kupungunza tatizo la foleni katika barabara ya morogoro.
Rais Kikwete aliwasili katika kijiji cha kiwangwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa kilometa 64 za barabara ya  msata –bagamoyo kwa kiwango cha lami na akatumia fursa hiyo kuwaasa wakazi wa mkoa wa Pwani kutumia barabara hiyo kujiletea maendeleo.
Halikadhalika Rais Kikwete amezungumzia tatizo la watu wanaovamia na kujenga nyumba katika hifadhi ya barabara kuwa katu hawatalipwa fidia na badala yake watakaolipwa fidia ni wale tu ambao watabainika kuwa barabara iliwakuta.
Mapema akimkaribisha Rais Kikwete kwenye sherehe hizo, waziri wa ujenzi Dokta John Magufuli ameiomba bodi ya wakandarasi nchini kuichukulia hatua kampuni  iliyopewa zabuni ya kufanyia tathmnini ujenzi wa barabara hiyo kwa kuifanya kwa kiwango cha chini jambo ambalo limeisababishia serikali hasara kubwa.
Mkuu wa wakala wa ujenzi wa barabara nchini injinia Patric Mfugale amesema ujenzi wa kilometa 64 za barabara ya Msata Bagamoyo unagharimu shilingi bilioni 90 fedha ambazo zimetolewa na serikali ya Tanzania ambapo hadi sasa kilometa 37 zimekamilika.

No comments:

Post a Comment