Enter Adress

Wednesday, October 17, 2012

Waziri Kigoda afungua maonesho ya biashara A. Mashariki



Waziri wa viwanda, biashara na masoko Dkt.Abdala Kigoda amefungua maonyesho ya saba ya biashara ya afrika mashariki yanayofanyika jijini Mwanza.
Katika ufunguzi huo, Waziri kigoda amebainisha azma ya nchi za jumuiya ya afrika mashariki ya kuanzisha vituo maalum vya ukaguzi wa bidhaa katika maeneo ya mipaka ili kuwaondolea wafanyabiashara upotevu wa muda na usumbufu wanaoupata hivi sasa wanaposafirisha bidhaa zao kutoka nchi moja kwenda nyingine.
Dkt.Kigoda amesema kuwa vituo hivyo vitakavyojulikana kwa jina la one border post center vitawawezesha wafanyabiashara wanaoingiza ama kutoa bidhaa zao nchini kukaguliwa katika kituo kimoja pekee tofauti na sasa ambapo wafanyabiashara wanakumbana na vikwazo mbalimbali vikiwemo idadi kubwa ya vizuizi vilivyoko barabarani.
Ni maonyesho ya saba ya biashara ya afrika mashariki yanayofanyika jijini mwanza na kushirikisha makampuni na taasisi mbalimbali za kibiashara kutoka nchi za Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na wenyeji Tanzania.
Waziri Kigoda pia ameletoa rai kuwa maonyesho hayo yatumike kuondoa dhana potofu iliyojengeka miongoni mwa wananchi kuwa bidhaa bora ni zile zinazotoka nje ya jumuiya ya afrika mashariki.
Maonyesho hayo yanayozishirikisha zaidi ya makampuni mia nne kutoka ndani na nje ya nchi yanatarajia kufikia tamati Septemba tisa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment